Sheria na Masharti ya Ziada ya Watumiaji wa Hatima wa Ramani za Google
Mara ya Mwisho Kurekebishwa: Tarehe 4 Juni, 2025
Kwa kutumia Ramani za Google au bidhaa na huduma zozote za washirika wengine zilizojumuishwa kwenye Huduma za Jukwaa la Ramani za Google, wewe, ukiwa mtumiaji wa hatima, ni sharti ukubali (1) Sheria na Masharti ya Google na (2) Sheria na Masharti haya ya Ziada ya Ramani za Google (“Masharti ya Ziada ya Ramani”). Masharti ya Ziada ya Ramani yanajumuisha kwa marejeleo Ilani za Kisheria kuhusu Ramani za Google au Google Earth na API za Ramani za Google au Google Earth.
Tafadhali soma kwa makini hati hizi zote. Kwa pamoja, hati hizi zinajulikana kama “Sheria na Masharti”. Zinabainisha kile unachoweza kutarajia kutoka kwetu na tunachotarajia kutoka kwako unapotumia huduma zetu.
Ikiwa unatumia vipengele vya wauzaji pekee katika Ramani za Google kudhibiti Wasifu wako wa Biashara, basi Sheria na Masharti ya Wasifu wa Biashara kwenye Google yaliyo katika https://support.google.com/business/answer/9292476 yatatumika.
Tunakuhimiza usome Sera yetu ya Faragha. Inaelezea taarifa tunazokusanya, sababu ya kuzikusanya na jinsi unaweza kubadilisha, kudhibiti, kuhamisha na kufuta taarifa zako.
Leseni. Ilimradi unatii Sheria na Masharti haya, Sheria na Masharti ya Google yanakupa leseni ya kutumia Ramani za Google, vikiwemo vipengele vinavyokuruhusu:
uangalie na uweke vidokezo kwenye ramani;
uunde faili za KML na uweke safu kwenye ramani; na
uonyeshe hadharani maudhui yaliyo na maelezo sahihi mtandaoni, kwenye video na machapisho.
Tafadhali angalia ukurasa wa ruhusa ya ukitumia Ramani za Google, Google Earth na Taswira ya Mtaa ili upate maelezo zaidi kuhusu mambo mahususi unayoruhusiwa kufanya kwenye Ramani za Google.
Matumizi Yaliyopigwa Marufuku. Kutii Kifungu hiki cha 2 ni sharti la kupata leseni yako ya kutumia Ramani za Google. Unapotumia Ramani za Google, huruhusiwi (au hupaswi kuwaruhusu wanaokuwakilisha):
kusambaza au kuuza sehemu yoyote ya Ramani za Google au kutayarisha bidhaa au huduma mpya inayotokana na Ramani za Google;
kunakili maudhui (isipokuwa uwe umeruhusiwa kufanya hivyo kulingana na ukurasa wa ruhusa za ukitumia Ramani za Google, Google Earth na Taswira ya Mtaa au sheria ya haki za uvumbuzi inayotumika, ikiwa ni pamoja na "matumizi ya haki");
kupakua kwa wingi au kuanzisha mipasho mingi ya maudhui (au kumruhusu mtu mwingine yeyote afanye hivyo);
kutumia Ramani za Google kutayarisha au kukuza seti nyingine yoyote ya data inayohusiana na ramani (ikiwa ni pamoja na seti ya data ya ramani au uelekezaji, hifadhidata ya orodha za biashara, orodha ya wanaopokea barua pepe au orodha ya utangazaji kwa kutumia simu) ya kutumiwa katika huduma mbadala au huduma inayofanana kwa karibu na Ramani za Google; au
kutumia sehemu yoyote ya Ramani za Google pamoja na bidhaa au huduma za watu wengine kwa kusudi au kuhusiana na uelekezaji au udhibiti wa gari linalojiendesha katika wakati halisi, isipokuwa kupitia kipengele mahususi kinachotolewa na Google kama vile Android Auto.
Hali Halisi; Kukubali Hatari. Unapotumia data ya ramani, hali ya msongamano wa magari, maelekezo na maudhui mengine ya Ramani za Google, unaweza kuona kuwa hali halisi inatofautiana na matokeo ya ramani na maudhui, kwa hivyo fanya uamuzi wako binafsi au utumie Ramani za Google kwa wajibu wako mwenyewe. Unawajibikia jinsi unatumia huduma hizi na matokeo ya matumizi hayo, wakati wote.
Maudhui Yako kwenye Ramani za Google. Maudhui unayopakia, kuwasilisha, kuhifadhi, kutuma au kupokea kupitia Ramani za Google yanapaswa kutii Sheria na Masharti ya Google, ikiwa ni pamoja na leseni katika kifungu cha “Ruhusa ya kutumia maudhui yako”. Hata hivyo, maudhui yanayosalia tu kwenye kifaa chako (kama vile faili ya KML iliyohifadhiwa kwenye kifaa chako) hayapakiwi wala kutumwa kwa Google. Kwa hivyo, hayasimamiwi na leseni hiyo.
Watumiaji wa Hatima wa Serikali. Ikiwa unatumia Ramani za Google kama mwakilishi wa asasi ya serikali, sheria na masharti yafuatayo yanatumika:
Sheria Inayoongoza.
- Kwa asasi za serikali za jiji au jimbo nchini Marekani na Umoja wa Ulaya, kifungu cha Sheria na Masharti ya Google kinachohusiana na sheria inayoongoza na mahala pa kesi hakitatumika.
- Kwa asasi za serikali za Marekani, kifungu cha Sheria na Masharti ya Google kinachohusiana na sheria inayoongoza na mahala pa kesi hakitatumiwa na badala yake tutatumia kifungu kifuatacho: “Sheria na Masharti haya yatasimamiwa, kufasiriwa na kutekelezwa kwa mujibu wa sheria za Marekani bila kurejelea migongano ya kisheria. Kwa kiasi kinachoruhusiwa na sheria ya nchi ya Marekani: (A) sheria za Jimbo la California (isipokuwa kanuni za migongano ya kisheria za California) zitatumika pale ambapo sheria husika za serikali ya nchi hazipo; na (B) mzozo wowote unaotokana au unaohusiana na Sheria na Masharti haya ya Ramani za Google utashughulikiwa tu katika mahakama za serikali za Kaunti ya Santa Clara, California, na wahusika wote wakubali eneo la mamlaka binafsi katika mahakama hizo.”
Haki Zinazodhibitiwa za Serikali ya Marekani. Ufikiaji au utumiaji wote wa Ramani za Google unaotekelezwa na serikali ya nchi ya Marekani au kwa niaba yake, unapaswa kutii kifungu cha "Haki Zinazodhibitiwa za Serikali ya Marekani" katika Ilani za Kisheria za Ramani za Google au Google Earth.